Agano la Kale

Agano Jipya

Yn. 1:4-15 Swahili Union Version (SUV)

4. Ndani yake ndimo ulimokuwa uzima, nao ule uzima ulikuwa nuru ya watu.

5. Nayo nuru yang’aa gizani, wala giza halikuiweza.

6. Palitokea mtu, ametumwa kutoka kwa Mungu, jina lake Yohana.

7. Huyo alikuja kwa ushuhuda, ili aishuhudie ile nuru, wote wapate kuamini kwa yeye.

8. Huyo hakuwa ile nuru, bali alikuja ili aishuhudie ile nuru.

9. Kulikuwako Nuru halisi, amtiaye nuru kila mtu, akija katika ulimwengu.

10. Alikuwako ulimwenguni, hata kwa yeye ulimwengu ulipata kuwako, wala ulimwengu haukumtambua.

11. Alikuja kwake, wala walio wake hawakumpokea.

12. Bali wote waliompokea aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa Mungu, ndio wale waliaminio jina lake;

13. waliozaliwa, si kwa damu, wala si kwa mapenzi ya mwili, wala si kwa mapenzi ya mtu, bali kwa Mungu.

14. Naye Neno alifanyika mwili, akakaa kwetu; nasi tukauona utukufu wake, utukufu kama wa Mwana pekee atokaye kwa Baba; amejaa neema na kweli.

15. Yohana alimshuhudia, akapaza sauti yake akasema, Huyu ndiye niliyenena habari zake ya kwamba, Ajaye nyuma yangu amekuwa mbele yangu; kwa maana alikuwa kabla yangu.

Kusoma sura kamili Yn. 1