Agano la Kale

Agano Jipya

Yn. 1:32-37 Swahili Union Version (SUV)

32. Tena Yohana akashuhudia akisema, Nimemwona Roho akishuka kama hua kutoka mbinguni; naye akakaa juu yake.

33. Wala mimi sikumjua; lakini yeye aliyenipeleka kubatiza kwa maji, huyo aliniambia, Yeye ambaye utamwona Roho akishuka na kukaa juu yake, huyo ndiye abatizaye kwa Roho Mtakatifu.

34. Nami nimeona, tena nimeshuhudia ya kuwa huyu ni Mwana wa Mungu.

35. Tena siku ya pili yake Yohana alikuwa amesimama pamoja na wawili katika wanafunzi wake.

36. Akamtazama Yesu akitembea, akasema, Tazama, Mwana-kondoo wa Mungu!

37. Wale wanafunzi wawili wakamsikia akinena, wakamfuata Yesu.

Kusoma sura kamili Yn. 1