1. Hapo mwanzo kulikuwako Neno, naye Neno alikuwako kwa Mungu, naye Neno alikuwa Mungu.
2. Huyo mwanzo alikuwako kwa Mungu.
3. Vyote vilifanyika kwa huyo; wala pasipo yeye hakikufanyika cho chote kilichofanyika.
4. Ndani yake ndimo ulimokuwa uzima, nao ule uzima ulikuwa nuru ya watu.