Agano la Kale

Agano Jipya

Ufu. 8:1-6 Swahili Union Version (SUV)

1. Hata alipoifungua muhuri ya saba, kukawa kimya mbinguni kama muda wa nusu saa.

2. Nami nikawaona wale malaika saba wasimamao mbele za Mungu, nao wakapewa baragumu saba.

3. Na malaika mwingine akaja akasimama mbele ya madhabahu, mwenye chetezo cha dhahabu, akapewa uvumba mwingi, ili autie pamoja na maombi ya watakatifu wote juu ya madhabahu ya dhahabu, iliyo mbele ya kiti cha enzi.

4. Na moshi wa ule uvumba ukapanda mbele za Mungu pamoja na maombi ya watakatifu, kutoka mkononi mwa malaika.

5. Na huyo malaika akakitwaa kile chetezo, akakijaza moto wa madhabahu, akautupa juu ya nchi, kukawa radi na sauti na umeme na tetemeko la nchi.

6. Na wale malaika saba wenye baragumu saba wakajifanya tayari ili wazipige.

Kusoma sura kamili Ufu. 8