Agano la Kale

Agano Jipya

Ufu. 7:1-5 Swahili Union Version (SUV)

1. Baada ya hayo nikaona malaika wanne wamesimama katika pembe nne za nchi, wakizizuia pepo nne za nchi, upepo usivume juu ya nchi, wala juu ya bahari, wala juu ya mti wo wote.

2. Nikaona malaika mwingine, akipanda kutoka maawio ya jua, mwenye muhuri ya Mungu aliye hai; akawapigia kelele kwa sauti kuu wale malaika wanne waliopewa kuidhuru nchi na bahari,

3. akisema, Msiidhuru nchi, wala bahari, wala miti, hata tutakapokwisha kuwatia muhuri watumwa wa Mungu wetu juu ya vipaji vya nyuso zao.

4. Nikasikia hesabu yao waliotiwa muhuri katika kila kabila ya Waisraeli, watu mia na arobaini na nne elfu.

5. Wa kabila ya Yuda kumi na mbili elfu waliotiwa muhuri.Wa kabila ya Reubeni kumi na mbili elfu.Wa kabila ya Gadi kumi na mbili elfu.

Kusoma sura kamili Ufu. 7