Agano la Kale

Agano Jipya

Ufu. 3:10-13 Swahili Union Version (SUV)

10. Kwa kuwa umelishika neno la subira yangu, mimi nami nitakulinda, utoke katika saa ya kuharibiwa iliyo tayari kuujilia ulimwengu wote, kuwajaribu wakaao juu ya nchi.

11. Naja upesi. Shika sana ulicho nacho, asije mtu akaitwaa taji yako.

12. Yeye ashindaye, nitamfanya kuwa nguzo katika hekalu la Mungu wangu, wala hatatoka humo tena kabisa, nami nitaandika juu yake jina la Mungu wangu, na jina la mji wa Mungu wangu, huo Yerusalemu mpya, ushukao kutoka mbinguni kwa Mungu wangu, na jina langu mwenyewe, lile jipya.

13. Yeye aliye na sikio, na alisikie neno hili ambalo Roho ayaambia makanisa.

Kusoma sura kamili Ufu. 3