Agano la Kale

Agano Jipya

Ufu. 2:21-25 Swahili Union Version (SUV)

21. Nami nimempa muda ili atubu, wala hataki kuutubia uzinzi wake.

22. Tazama, nitamtupa juu ya kitanda, na hao wazinio pamoja naye, wapate dhiki kubwa wasipotubia matendo yake;

23. nami nitawaua watoto wake kwa mauti. Na makanisa yote watajua ya kuwa mimi ndiye achunguzaye viuno na mioyo. Nami nitampa kila mmoja wenu kwa kadiri ya matendo yake.

24. Lakini nawaambia ninyi wengine mlioko Thiatira, wo wote wasio na mafundisho hayo, wasiozijua fumbo za Shetani, kama vile wasemavyo, Sitaweka juu yenu mzigo mwingine.

25. Ila mlicho nacho kishikeni sana, hata nitakapokuja.

Kusoma sura kamili Ufu. 2