Agano la Kale

Agano Jipya

Mdo 26:29-32 Swahili Union Version (SUV)

29. Paulo akamjibu, Namwomba Mungu kwamba, ikiwa kwa machache au ikiwa kwa mengi, si wewe tu ila na hao wote wanaonisikia leo wawe kama mimi, isipokuwa vifungo hivi.

30. Mfalme na liwali na Bernike na wale walioketi pamoja nao wakasimama;

31. hata walipoondoka wakasemezana, wakisema, Mtu huyu hatendi neno linalostahili kifo wala kufungwa.

32. Agripa akamwambia Festo, Mtu huyo angeweza kufunguliwa, kama asingalitaka rufani kwa Kaisari.

Kusoma sura kamili Mdo 26