Agano la Kale

Agano Jipya

Mdo 2:24-34 Swahili Union Version (SUV)

24. ambaye Mungu alimfufua, akiufungua uchungu wa mauti, kwa sababu haikuwezekana ashikwe nao.

25. Maana Daudi ataja habari zake,Nalimwona Bwana mbele yangu siku zote,Kwa kuwa yuko upande wa mkono wangu wa kuume, nisitikisike.

26. Kwa hiyo moyo wangu ukapendezewa,ulimi wangu ukafurahi;Tena mwili wangu nao utakaa katika matumaini.

27. Kwa maana hutaiacha roho yangu katika kuzimu;Wala hutamtoa Mtakatifu wako aone uharibifu.

28. Umenijuvisha njia za uzima;Utanijaza furaha kwa uso wako.

29. Waume, ndugu zangu, mniwie radhi, niseme kwa ujasiri mbele yenu habari za baba yetu mkuu, Daudi, ya kuwa alifariki akazikwa, na kaburi lake liko kwetu hata leo.

30. Basi kwa kuwa ni nabii, akijua ya kuwa Mungu amemwapia kwa kiapo, ya kwamba katika uzao wa viuno vyake atamketisha mmoja katika kiti chake cha enzi;

31. yeye mwenyewe akitangulia kuyaona haya, alitaja habari za kufufuka kwake Kristo, ya kwamba roho yake haikuachwa kuzimu, wala mwili wake haukuona uharibifu.

32. Yesu huyo Mungu alimfufua, na sisi sote tu mashahidi wake.

33. Basi yeye, akiisha kupandishwa hata mkono wa kuume wa Mungu, na kupokea kwa Baba ile ahadi ya Roho Mtakatifu, amekimwaga kitu hiki mnachokiona sasa na kukisikia.

34. Maana Daudi hakupanda mbinguni; bali yeye mwenyewe anasema,Bwana alimwambia Bwana wangu,Keti upande wa mkono wangu wa kuume.

Kusoma sura kamili Mdo 2