Agano la Kale

Agano Jipya

Mdo 12:12-16 Swahili Union Version (SUV)

12. Na alipokuwa akifikiri haya akafika nyumbani kwa Mariamu, mamaye Yohana, ambaye jina lake la pili ni Marko; na watu wengi walikuwa wamekutana humo wakiomba.

13. Naye alipobisha kilango cha lango, kijakazi, jina lake Roda, akaja kusikiliza.

14. Alipoitambua sauti ya Petro, hakukifungua lango, kwa ajili ya furaha, bali alipiga mbio, akaingia ndani akawaambia kwamba Petro anasimama mbele ya lango.

15. Wakamwambia, Una wazimu. Lakini yeye akakaza sana, akasema ya kwamba ndivyo hivyo. Wakanena, Ni malaika wake.

16. Petro akafuliza kugonga, hata walipokwisha kumfungulia wakamwona, wakastaajabu.

Kusoma sura kamili Mdo 12