Agano la Kale

Agano Jipya

Gal. 5:16-21 Swahili Union Version (SUV)

16. Basi nasema, Enendeni kwa Roho, wala hamtazitimiza kamwe tamaa za mwili.

17. Kwa sababu mwili hutamani ukishindana na Roho, na Roho kushindana na mwili; kwa maana hizi zimepingana, hata hamwezi kufanya mnayotaka.

18. Lakini mkiongozwa na Roho, hampo chini ya sheria.

19. Basi matendo ya mwili ni dhahiri, ndiyo haya, uasherati, uchafu, ufisadi,

20. ibada ya sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, fitina, faraka, uzushi,

21. husuda, ulevi, ulafi, na mambo yanayofanana na hayo, katika hayo nawaambia mapema, kama nilivyokwisha kuwaambia, ya kwamba watu watendao mambo ya jinsi hiyo hawataurithi ufalme wa Mungu.

Kusoma sura kamili Gal. 5