Agano la Kale

Agano Jipya

Gal. 5:1-15 Swahili Union Version (SUV)

1. Katika ungwana huo Kristo alituandika huru; kwa hiyo simameni, wala msinaswe tena chini ya kongwa la utumwa.

2. Tazama, mimi Paulo nawaambia ninyi ya kwamba, mkitahiriwa, Kristo hatawafaidia neno.

3. Tena namshuhudia kila mtu atahiriwaye, kwamba ni wajibu wake kuitimiza torati yote.

4. Mmetengwa na Kristo, ninyi mtakao kuhesabiwa haki kwa sheria; mmeanguka na kutoka katika hali ya neema.

5. Maana sisi kwa Roho tunalitazamia tumaini la haki kwa njia ya imani.

6. Maana katika Kristo Yesu kutahiriwa hakufai neno, wala kutokutahiriwa, bali imani itendayo kazi kwa upendo.

7. Mlikuwa mkipiga mbio vizuri; ni nani aliyewazuia msiitii kweli?

8. Kushawishi huku hakukutoka kwake yeye anayewaita ninyi.

9. Chachu kidogo huchachua donge zima.

10. Nina matumaini kwenu katika Bwana, ya kwamba hamtakuwa na nia ya namna nyingine. Lakini yeye anayewafadhaisha atachukua hukumu yake, awaye yote.

11. Nami, ndugu zangu ikiwa ninahubiri habari ya kutahiriwa, kwa nini ningali ninaudhiwa? Hapo kwazo la msalaba limebatilika!

12. Laiti hao wanaowatia mashaka wangejikata nafsi zao!

13. Maana ninyi, ndugu, mliitwa mpate uhuru; lakini uhuru wenu usiwe sababu ya kuufuata mwili, bali tumikianeni kwa upendo.

14. Maana torati yote imetimilika katika neno moja, nalo ni hili, Umpende jirani yako kama nafsi yako.

15. Lakini mkiumana na kulana, angalieni msije mkaangamizana.

Kusoma sura kamili Gal. 5