Agano la Kale

Agano Jipya

Gal. 3:3-10 Swahili Union Version (SUV)

3. Je! Mmekuwa wajinga namna hii? Baada ya kuanza katika Roho, mnataka kukamilishwa sasa katika mwili?

4. Mmepatikana na mateso makubwa namna hii bure? Ikiwa ni bure kweli.

5. Basi, yeye awapaye Roho na kufanya miujiza kati yenu, je! Afanya hayo kwa matendo ya sheria, au kwa kusikia kunakotokana na imani?

6. Kama vile Ibrahimu alivyomwamini Mungu akahesabiwa haki.

7. Fahamuni basi, ya kuwa wale walio wa imani, hao ndio wana wa Ibrahimu.

8. Na andiko, kwa vile lilivyoona tangu zamani kwamba Mungu atawahesabia haki Mataifa kwa imani, lilimhubiri Ibrahimu habari njema zamani, kusema, Katika wewe Mataifa yote watabarikiwa.

9. Basi hao walio wa imani hubarikiwa pamoja na Ibrahimu aliyekuwa mwenye imani.

10. Kwa maana wale wote walio wa matendo ya sheria, wako chini ya laana; maana imeandikwa, Amelaaniwa kila mtu asiyedumu katika yote yaliyoandikwa katika kitabu cha torati, ayafanye.

Kusoma sura kamili Gal. 3