Agano la Kale

Agano Jipya

Gal. 3:20-27 Swahili Union Version (SUV)

20. Basi aliye mjumbe si mjumbe wa mmoja; bali Mungu ni mmoja.

21. Basi je! Torati haipatani na ahadi za Mungu? Hasha! Kwa kuwa, kama ingalitolewa sheria iwezayo kuhuisha, yakini haki ingalipatikana kwa sheria.

22. Lakini andiko limeyafunga yote chini ya nguvu ya dhambi, makusudi hao waaminio wapewe ile ahadi kwa imani ya Yesu Kristo.

23. Lakini kabla ya kuja ile imani tulikuwa tumewekwa chini ya sheria, tumefungwa mpaka ije ile imani itakayofunuliwa.

24. Hivyo torati imekuwa kiongozi kutuleta kwa Kristo, ili tuhesabiwe haki kwa imani.

25. Lakini, iwapo imani imekuja, hatupo tena chini ya kiongozi.

26. Kwa kuwa ninyi nyote mmekuwa wana wa Mungu kwa njia ya imani katika Kristo Yesu.

27. Maana ninyi nyote mliobatizwa katika Kristo mmemvaa Kristo.

Kusoma sura kamili Gal. 3