Agano la Kale

Agano Jipya

Gal. 3:1-8 Swahili Union Version (SUV)

1. Enyi Wagalatia msio na akili, ni nani aliyewaloga, ninyi ambao Yesu Kristo aliwekwa wazi mbele ya macho yenu ya kuwa amesulibiwa?

2. Nataka kujifunza neno hili moja kwenu. Je! Mlipokea Roho kwa matendo ya sheria, au kwa kusikia kunakotokana na imani?

3. Je! Mmekuwa wajinga namna hii? Baada ya kuanza katika Roho, mnataka kukamilishwa sasa katika mwili?

4. Mmepatikana na mateso makubwa namna hii bure? Ikiwa ni bure kweli.

5. Basi, yeye awapaye Roho na kufanya miujiza kati yenu, je! Afanya hayo kwa matendo ya sheria, au kwa kusikia kunakotokana na imani?

6. Kama vile Ibrahimu alivyomwamini Mungu akahesabiwa haki.

7. Fahamuni basi, ya kuwa wale walio wa imani, hao ndio wana wa Ibrahimu.

8. Na andiko, kwa vile lilivyoona tangu zamani kwamba Mungu atawahesabia haki Mataifa kwa imani, lilimhubiri Ibrahimu habari njema zamani, kusema, Katika wewe Mataifa yote watabarikiwa.

Kusoma sura kamili Gal. 3