Agano la Kale

Agano Jipya

Ebr. 7:9-12 Swahili Union Version (SUV)

9. Tena yaweza kusemwa ya kuwa, kwa njia ya Ibrahimu, hata Lawi apokeaye sehemu ya kumi alitoa sehemu ya kumi;

10. kwa maana alikuwa katika viuno vya baba yake, hapo Melkizedeki alipokutana naye.

11. Basi, kama ukamilifu ulikuwapo kwa ukuhani wa Lawi; (maana watu wale waliipata sheria kwa huo); kulikuwa na haja gani tena ya kuhani mwingine ainuke, kwa mfano wa Melkizedeki, wala asihesabiwe kwa mfano wa Haruni?

12. Maana ukuhani ule ukibadilika, hapana budi sheria nayo ibadilike.

Kusoma sura kamili Ebr. 7