Agano la Kale

Agano Jipya

Ebr. 7:22-28 Swahili Union Version (SUV)

22. basi kwa kadiri hii Yesu amekuwa mdhamini wa agano lililo bora zaidi.

23. Tena wale walifanywa makuhani wengi, kwa sababu wazuiliwa na mauti wasikae;

24. bali yeye, kwa kuwa akaa milele, anao ukuhani wake usioondoka.

25. Naye, kwa sababu hii, aweza kuwaokoa kabisa wao wamjiao Mungu kwa yeye; maana yu hai sikuzote ili awaombee.

26. Maana ilitupasa sisi tuwe na kuhani mkuu wa namna hii aliye mtakatifu, asiyekuwa na uovu, asiyekuwa na waa lo lote, aliyetengwa na wakosaji, aliyekuwa juu kuliko mbingu;

27. ambaye hana haja kila siku, mfano wa wale makuhani wakuu wengine, kwanza kutoa dhabihu kwa ajili ya dhambi zake mwenyewe, kisha kwa ajili ya dhambi za hao watu; maana yeye alifanya hivi mara moja, alipojitoa nafsi yake.

28. Maana torati yawaweka wanadamu walio na unyonge kuwa makuhani wakuu; bali hilo neno la kiapo kilichokuja baada ya torati limemweka Mwana, aliyekamilika hata milele.

Kusoma sura kamili Ebr. 7