Agano la Kale

Agano Jipya

Ebr. 7:19-24 Swahili Union Version (SUV)

19. (kwa maana ile sheria haikukamilisha neno); na pamoja na hayo kuliingizwa matumaini yaliyo mazuri zaidi, ambayo kwa hayo twamkaribia Mungu.

20. Na kwa kuwa haikuwa pasipo kiapo,

21. (maana wale walifanywa makuhani pasipo kiapo; bali yeye, pamoja na kiapo, kwa yeye aliyemwambia,Bwana ameapa wala hataghairi,Wewe u kuhani milele;)

22. basi kwa kadiri hii Yesu amekuwa mdhamini wa agano lililo bora zaidi.

23. Tena wale walifanywa makuhani wengi, kwa sababu wazuiliwa na mauti wasikae;

24. bali yeye, kwa kuwa akaa milele, anao ukuhani wake usioondoka.

Kusoma sura kamili Ebr. 7