19. (kwa maana ile sheria haikukamilisha neno); na pamoja na hayo kuliingizwa matumaini yaliyo mazuri zaidi, ambayo kwa hayo twamkaribia Mungu.
20. Na kwa kuwa haikuwa pasipo kiapo,
21. (maana wale walifanywa makuhani pasipo kiapo; bali yeye, pamoja na kiapo, kwa yeye aliyemwambia,Bwana ameapa wala hataghairi,Wewe u kuhani milele;)
22. basi kwa kadiri hii Yesu amekuwa mdhamini wa agano lililo bora zaidi.
23. Tena wale walifanywa makuhani wengi, kwa sababu wazuiliwa na mauti wasikae;
24. bali yeye, kwa kuwa akaa milele, anao ukuhani wake usioondoka.