Agano la Kale

Agano Jipya

Ebr. 7:14-25 Swahili Union Version (SUV)

14. Maana ni dhahiri kwamba Bwana wetu alitoka katika Yuda, kabila ambayo Musa hakunena neno lo lote juu yake katika mambo ya ukuhani.

15. Tena hayo tusemayo ni dhahiri sana zaidi, ikiwa ametokea kuhani mwingine mithili ya Melkizedeki;

16. asiyekuwa kuhani kwa sheria ya amri iliyo ya jinsi ya mwili, bali kwa nguvu za uzima usio na ukomo;

17. maana ameshuhudiwa kwamba,Wewe u kuhani mileleKwa mfano wa Melkizedeki.

18. Maana, kuna kubatiliwa kwa ile amri iliyotangulia, kwa sababu ya udhaifu wake, na kutokufaa kwake;

19. (kwa maana ile sheria haikukamilisha neno); na pamoja na hayo kuliingizwa matumaini yaliyo mazuri zaidi, ambayo kwa hayo twamkaribia Mungu.

20. Na kwa kuwa haikuwa pasipo kiapo,

21. (maana wale walifanywa makuhani pasipo kiapo; bali yeye, pamoja na kiapo, kwa yeye aliyemwambia,Bwana ameapa wala hataghairi,Wewe u kuhani milele;)

22. basi kwa kadiri hii Yesu amekuwa mdhamini wa agano lililo bora zaidi.

23. Tena wale walifanywa makuhani wengi, kwa sababu wazuiliwa na mauti wasikae;

24. bali yeye, kwa kuwa akaa milele, anao ukuhani wake usioondoka.

25. Naye, kwa sababu hii, aweza kuwaokoa kabisa wao wamjiao Mungu kwa yeye; maana yu hai sikuzote ili awaombee.

Kusoma sura kamili Ebr. 7