Agano la Kale

Agano Jipya

Ebr. 4:1-10 Swahili Union Version (SUV)

1. Basi, ikiwa ikaliko ahadi ya kuingia katika raha yake, na tuogope, mmoja wenu asije akaonekana ameikosa.

2. Maana ni kweli, sisi nasi tumehubiriwa habari njema vile vile kama hao. Lakini neno lile lililosikiwa halikuwafaa hao, kwa sababu halikuchanganyika na imani ndani yao waliosikia.

3. Maana sisi tulioamini tunaingia katika raha ile; kama vile alivyosema,Kama nilivyoapa kwa hasira yangu,Hawataingia rahani mwangu:ijapokuwa zile kazi zilimalizika tangu kuwekwa misingi ya ulimwengu.

4. Kwa maana ameinena siku ya saba mahali fulani hivi, Mungu alistarehe siku ya saba, akaziacha kazi zake zote;

5. na hapa napo, Hawataingia rahani mwangu.

6. Basi, kwa kuwa neno hili limebaki kwamba wako watu watakaoingia humo, na wale waliohubiriwa habari ile zamani walikosa kuingia kwa sababu ya kuasi kwao,

7. aweka tena siku fulani, akisema katika Daudi baada ya muda mwingi namna hii, Leo; kama ilivyonenwa tangu zamani,Leo, kama mtaisikia sauti yake,Msifanye migumu mioyo yenu.

8. Maana kama Yoshua angaliwapa raha, asingaliinena siku nyingine baadaye.

9. Basi, imesalia raha ya sabato kwa watu wa Mungu.

10. Kwa maana yeye aliyeingia katika raha yake amestarehe mwenyewe katika kazi yake, kama vile Mungu alivyostarehe katika kazi zake.

Kusoma sura kamili Ebr. 4