Agano la Kale

Agano Jipya

Ebr. 2:5-9 Swahili Union Version (SUV)

5. Maana hakuuweka chini ya malaika ulimwengu ule ujao tunaounena, ila mtu mmoja ameshuhudia hivi mahali fulani, akisema,

6. Mwanadamu ni nini hata umkumbuke,Ama mwana wa binadamu, hata umwangalie?

7. Umemfanya mdogo punde kuliko malaika,Umemvika taji ya utukufu na heshima,Umemtawaza juu ya kazi za mikono yako;

8. Umeweka vitu vyote chini ya nyayo zake.Kwa maana katika kuweka vitu vyote chini yake hakusaza kitu kisichowekwa chini yake. Lakini sasa bado hamjaona vitu vyote kutiwa chini yake,

9. ila twamwona yeye aliyefanywa mdogo punde kuliko malaika, yaani, Yesu, kwa sababu ya maumivu ya mauti, amevikwa taji ya utukufu na heshima, ili kwa neema ya Mungu aionje mauti kwa ajili ya kila mtu.

Kusoma sura kamili Ebr. 2