Agano la Kale

Agano Jipya

Ebr. 13:11-14 Swahili Union Version (SUV)

11. Maana wanyama wale ambao damu yao huletwa ndani ya patakatifu na kuhani mkuu kwa ajili ya dhambi, viwiliwili vyao huteketezwa nje ya kambi.

12. Kwa ajili hii Yesu naye, ili awatakase watu kwa damu yake mwenyewe, aliteswa nje ya lango.

13. Basi na tutoke tumwendee nje ya kambi, tukichukua shutumu lake.

14. Maana hapa hatuna mji udumuo, bali twautafuta ule ujao.

Kusoma sura kamili Ebr. 13