Agano la Kale

Agano Jipya

Ebr. 11:29-32 Swahili Union Version (SUV)

29. Kwa imani wakapita kati ya Bahari ya Shamu, kama katika nchi kavu; Wamisri walipojaribu kufanya vivyo wakatoswa.

30. Kwa imani kuta za Yeriko zikaanguka, zilipokwisha kuzungukwa siku saba.

31. Kwa imani Rahabu, yule kahaba, hakuangamia pamoja na hao walioasi; kwa kuwa aliwakaribisha wale wapelelezi kwa amani.

32. Nami niseme nini tena? Maana wakati usingenitosha kuleta habari za Gideoni na Baraka na Samsoni na Yeftha na Daudi na Samweli na za manabii;

Kusoma sura kamili Ebr. 11