Agano la Kale

Agano Jipya

Ebr. 10:8-16 Swahili Union Version (SUV)

8. Hapo juu asemapo, Dhabihu na matoleo na sadaka za kuteketezwa na hizo za dhambi hukuzitaka, wala hukupendezwa nazo (zitolewazo kama ilivyoamuru torati),

9. ndipo aliposema, Tazama, nimekuja niyafanye mapenzi yako. Aondoa la kwanza, ili kusudi alisimamishe la pili.

10. Katika mapenzi hayo mmepata utakaso, kwa kutolewa mwili wa Yesu Kristo mara moja tu.

11. Na kila kuhani husimama kila siku akifanya ibada, na kutoa dhabihu zile zile mara nyingi; ambazo haziwezi kabisa kuondoa dhambi.

12. Lakini huyu, alipokwisha kutoa kwa ajili ya dhambi dhabihu moja idumuyo hata milele, aliketi mkono wa kuume wa Mungu;

13. tangu hapo akingojea hata adui zake wawekwe kuwa chini ya miguu yake.

14. Maana kwa toleo moja amewakamilisha hata milele hao wanaotakaswa.

15. Na Roho Mtakatifu naye amshuhudia; kwa maana, baada ya kusema,

16. Hili ni agano nitakaloagana nao baada ya siku zile, anena Bwana,Nitatia sheria zangu mioyoni mwao,Na katika nia zao nitaziandika;ndipo anenapo,

Kusoma sura kamili Ebr. 10