Agano la Kale

Agano Jipya

Ebr. 1:3-7 Swahili Union Version (SUV)

3. Yeye kwa kuwa ni mng’ao wa utukufu wake na chapa ya nafsi yake, akivichukua vyote kwa amri ya uweza wake, akiisha kufanya utakaso wa dhambi, aliketi mkono wa kuume wa Ukuu huko juu;

4. amefanyika bora kupita malaika, kwa kadiri jina alilolirithi lilivyo tukufu kuliko lao.

5. Kwa maana alimwambia malaika yupi wakati wo wote,Ndiwe mwanangu,Mimi leo nimekuzaa?Na tenaMimi nitakuwa kwake baba,Na yeye atakuwa kwangu mwana?

6. Hata tena, amletapo mzaliwa wa kwanza ulimwenguni, asema,Na wamsujudu malaika wote wa Mungu.

7. Na kwa habari za malaika asema,Afanyaye malaika wake kuwa pepo,Na watumishi wake kuwa miali ya moto.

Kusoma sura kamili Ebr. 1