Agano la Kale

Agano Jipya

1 Pet. 3:1-12 Swahili Union Version (SUV)

1. Kadhalika ninyi wake, watiini waume zenu; kusudi, ikiwa wako wasioliamini Neno, wavutwe kwa mwenendo wa wake zao, pasipo lile Neno;

2. wakiutazama mwenendo wenu safi, na wa hofu.

3. Kujipamba kwenu, kusiwe kujipamba kwa nje, yaani, kusuka nywele; na kujitia dhahabu, na kuvalia mavazi;

4. bali kuwe utu wa moyoni usioonekana, katika mapambo yasiyoharibika; yaani, roho ya upole na utulivu, iliyo ya thamani kuu mbele za Mungu.

5. Maana hivyo ndivyo walivyojipamba wanawake watakatifu wa zamani, waliomtumaini Mungu, na kuwatii waume zao.

6. Kama vile Sara alivyomtii Ibrahimu, akamwita Bwana; nanyi ni watoto wake, mfanyapo mema, wala hamkutishwa kwa hofu yo yote.

7. Kadhalika ninyi waume, kaeni na wake zenu kwa akili; na kumpa mke heshima, kama chombo kisicho na nguvu; na kama warithi pamoja wa neema ya uzima, kusudi kuomba kwenu kusizuiliwe.

8. Neno la mwisho ni hili; mwe na nia moja, wenye kuhurumiana, wenye kupendana kama ndugu, wasikitikivu, wanyenyekevu;

9. watu wasiolipa baya kwa baya, au laumu kwa laumu; bali wenye kubariki; kwa sababu hayo ndiyo mliyoitiwa ili mrithi baraka.

10. Kwa maana,Atakaye kupenda maisha,Na kuona siku njema,Auzuie ulimi wake usinene mabaya,Na midomo yake isiseme hila.

11. Na aache mabaya, atende mema;Atafute amani, aifuate sana.

12. Kwa kuwa macho ya Bwana huwaelekea wenye haki,Na masikio yake husikiliza maombi yao;Bali uso wa Bwana ni juu ya watenda mabaya.

Kusoma sura kamili 1 Pet. 3