Agano la Kale

Agano Jipya

1 Pet. 2:1-11 Swahili Union Version (SUV)

1. Basi, wekeni mbali uovu wote na hila yote, na unafiki na husuda na masingizio yote.

2. Kama watoto wachanga waliozaliwa sasa yatamanini maziwa ya akili yasiyoghoshiwa, ili kwa hayo mpate kuukulia wokovu;

3. ikiwa mmeonja ya kwamba Bwana ni mwenye fadhili.

4. Mmwendee yeye, jiwe lililo hai, lililokataliwa na wanadamu, bali kwa Mungu ni teule, lenye heshima.

5. Ninyi nanyi, kama mawe yaliyo hai, mmejengwa mwe nyumba ya Roho, ukuhani mtakatifu, mtoe dhabihu za roho, zinazokubaliwa na Mungu, kwa njia ya Yesu Kristo.

6. Kwa kuwa imeandikwa katika maandikoTazama, naweka katika Sayuni jiwe kuu la pembeni, teule, lenye heshima,Na kila amwaminiye hatatahayarika.

7. Basi, heshima hii ni kwenu ninyi mnaoamini. Bali kwao wasioamini,Jiwe walilolikataa waashi,Limekuwa jiwe kuu la pembeni.

8. Tena,Jiwe la kujikwaza mguu, na mwamba wa kuangusha.Kwa maana hujikwaza kwa neno lile, wasiliamini, nao waliwekwa kusudi wapate hayo.

9. Bali ninyi ni mzao mteule, ukuhani wa kifalme, taifa takatifu, watu wa milki ya Mungu, mpate kuzitangaza fadhili zake yeye aliyewaita mtoke gizani mkaingie katika nuru yake ya ajabu;

10. ninyi mliokuwa kwanza si taifa, bali sasa ni taifa la Mungu; mliokuwa hamkupata rehema, bali sasa mmepata rehema.

11. Wapenzi, nawasihi kama wapitaji na wasafiri, ziepukeni tamaa za mwili zipiganazo na roho.

Kusoma sura kamili 1 Pet. 2