Agano la Kale

Agano Jipya

1 Pet. 1:19-25 Swahili Union Version (SUV)

19. bali kwa damu ya thamani, kama ya mwana-kondoo asiye na ila, asiye na waa, yaani, ya Kristo.

20. Naye amejulikana kweli tangu zamani, kabla haijawekwa misingi ya dunia; lakini alifunuliwa mwisho wa zamani kwa ajili yenu;

21. ambao kwa yeye mmekuwa wenye kumwamini Mungu, aliyemfufua katika wafu akampa utukufu; hata imani yenu na tumaini lenu liwe kwa Mungu.

22. Mkiisha kujitakasa roho zenu kwa kuitii kweli, hata kuufikilia upendano wa ndugu usio na unafiki, basi jitahidini kupendana kwa moyo.

23. Kwa kuwa mmezaliwa mara ya pili; si kwa mbegu iharibikayo, bali kwa ile isiyoharibika; kwa neno la Mungu lenye uzima, lidumulo hata milele.

24. Maana,Mwili wote ni kama majani,Na fahari yake yote ni kama ua la majani.Majani hukauka na ua lake huanguka;

25. Bali Neno la Bwana hudumu hata milele.Na neno hilo ni neno lile jema lililohubiriwa kwenu.

Kusoma sura kamili 1 Pet. 1