13. Kwa hiyo vifungeni viuno vya nia zenu, na kuwa na kiasi; mkiitumainia kwa utimilifu ile neema mtakayoletewa katika ufunuo wake Yesu Kristo.
14. Kama watoto wa kutii msijifananishe na tamaa zenu za kwanza za ujinga wenu;
15. bali kama yeye aliyewaita alivyo mtakatifu, ninyi nanyi iweni watakatifu katika mwenendo wenu wote;
16. kwa maana imeandikwa, Mtakuwa watakatifu kwa kuwa mimi ni mtakatifu.