Agano la Kale

Agano Jipya

Zaburi 9:6-11 Biblia Habari Njema (BHN)

6. Maadui wameangamia milele;umeingolea mbali miji yao,kumbukumbu lao limetoweka.

7. Lakini Mwenyezi-Mungu anatawala milele;ameweka kiti chake cha enzi apate kuhukumu.

8. Anauhukumu ulimwengu kwa haki;anayaamua mataifa kwa unyofu.

9. Mwenyezi-Mungu ni ngome ya watu wanaoonewa;yeye ni ngome nyakati za taabu.

10. Wanaokujua wewe, ee Mungu hukutegemea,wewe Mwenyezi-Mungu huwatupi wakutafutao.

11. Mwimbieni sifa Mwenyezi-Mungu akaaye Siyoni.Yatangazieni mataifa mambo aliyotenda!

Kusoma sura kamili Zaburi 9