2. Nitafurahi na kushangilia kwa sababu yako;nitaliimbia sifa jina lako, ewe Mungu Mkuu.
3. Wakati ulipotokea, maadui zangu walirudi nyuma,walijikwaa na kuangamia.
4. Umenitetea kuhusu kisa changu cha haki;umeketi katika kiti chako cha enzi,ukatoa hukumu iliyo sawa.
5. Umeyakemea mataifa,umewaangamiza waovu;majina yao umeyafutilia mbali milele.
6. Maadui wameangamia milele;umeingolea mbali miji yao,kumbukumbu lao limetoweka.