Agano la Kale

Agano Jipya

Zaburi 9:12-20 Biblia Habari Njema (BHN)

12. Mungu hulipiza kisasi kwa umwagaji damu;kamwe hasahau kilio cha wanaoonewa.

13. Unirehemu, ee Mwenyezi-Mungu!Ona mateso ninayoteswa na wanaonichukia;wewe waninyakua kutoka nguvu za kifo,

14. nisimulie sifa zako mbele ya watu wa Siyoni,nipate kushangilia kwa sababu umeniokoa.

15. Watu wa mataifa wametumbukia katika shimo walilochimba,wamenaswa miguu katika wavu waliouficha.

16. Mwenyezi-Mungu amejionesha alivyo;ametekeleza hukumu.Watu waovu wamenaswa kwa matendo yao wenyewe.

17. Waovu wataishia kuzimu;naam, mataifa yote yanayomsahau Mungu.

18. Lakini fukara hawatasahauliwa daima;tumaini la maskini halitapotea milele.

19. Inuka, ee Mwenyezi-Mungu!Usimwache binadamu ashinde.Uyakusanye mataifa mbele yako, uyahukumu.

20. Uyatie hofu, ee Mwenyezi-Mungu,watu wa mataifa watambue kuwa wao ni watu tu!

Kusoma sura kamili Zaburi 9