10. Wanaokujua wewe, ee Mungu hukutegemea,wewe Mwenyezi-Mungu huwatupi wakutafutao.
11. Mwimbieni sifa Mwenyezi-Mungu akaaye Siyoni.Yatangazieni mataifa mambo aliyotenda!
12. Mungu hulipiza kisasi kwa umwagaji damu;kamwe hasahau kilio cha wanaoonewa.
13. Unirehemu, ee Mwenyezi-Mungu!Ona mateso ninayoteswa na wanaonichukia;wewe waninyakua kutoka nguvu za kifo,
14. nisimulie sifa zako mbele ya watu wa Siyoni,nipate kushangilia kwa sababu umeniokoa.