1. Nitakushukuru Mungu kwa moyo wangu wote;nitayasimulia matendo yako yote ya ajabu.
2. Nitafurahi na kushangilia kwa sababu yako;nitaliimbia sifa jina lako, ewe Mungu Mkuu.
3. Wakati ulipotokea, maadui zangu walirudi nyuma,walijikwaa na kuangamia.
4. Umenitetea kuhusu kisa changu cha haki;umeketi katika kiti chako cha enzi,ukatoa hukumu iliyo sawa.
5. Umeyakemea mataifa,umewaangamiza waovu;majina yao umeyafutilia mbali milele.
6. Maadui wameangamia milele;umeingolea mbali miji yao,kumbukumbu lao limetoweka.
7. Lakini Mwenyezi-Mungu anatawala milele;ameweka kiti chake cha enzi apate kuhukumu.
8. Anauhukumu ulimwengu kwa haki;anayaamua mataifa kwa unyofu.