Agano la Kale

Agano Jipya

Zaburi 9:1-12 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Nitakushukuru Mungu kwa moyo wangu wote;nitayasimulia matendo yako yote ya ajabu.

2. Nitafurahi na kushangilia kwa sababu yako;nitaliimbia sifa jina lako, ewe Mungu Mkuu.

3. Wakati ulipotokea, maadui zangu walirudi nyuma,walijikwaa na kuangamia.

4. Umenitetea kuhusu kisa changu cha haki;umeketi katika kiti chako cha enzi,ukatoa hukumu iliyo sawa.

5. Umeyakemea mataifa,umewaangamiza waovu;majina yao umeyafutilia mbali milele.

6. Maadui wameangamia milele;umeingolea mbali miji yao,kumbukumbu lao limetoweka.

7. Lakini Mwenyezi-Mungu anatawala milele;ameweka kiti chake cha enzi apate kuhukumu.

8. Anauhukumu ulimwengu kwa haki;anayaamua mataifa kwa unyofu.

9. Mwenyezi-Mungu ni ngome ya watu wanaoonewa;yeye ni ngome nyakati za taabu.

10. Wanaokujua wewe, ee Mungu hukutegemea,wewe Mwenyezi-Mungu huwatupi wakutafutao.

11. Mwimbieni sifa Mwenyezi-Mungu akaaye Siyoni.Yatangazieni mataifa mambo aliyotenda!

12. Mungu hulipiza kisasi kwa umwagaji damu;kamwe hasahau kilio cha wanaoonewa.

Kusoma sura kamili Zaburi 9