9. Uukomeshe uovu wa watu wabaya,uwaimarishe watu walio wema,ee Mungu uliye mwadilifu,uzijuaye siri za mioyo na fikira za watu.
10. Mungu ndiye ngao yangu;yeye huwaokoa wanyofu wa moyo.
11. Mungu ni hakimu wa haki;kila siku hulaumu maovu.
12. Watu wasipoongoka,Mungu atanoa upanga wake;atavuta upinde wake na kulenga shabaha.
13. Atatayarisha silaha zake za hatari,na kuipasha moto mishale yake.
14. Tazama! Mtu mbaya hutunga uovu,hujaa uharibifuna kuzaa udanganyifu.