Agano la Kale

Agano Jipya

Zaburi 7:9-14 Biblia Habari Njema (BHN)

9. Uukomeshe uovu wa watu wabaya,uwaimarishe watu walio wema,ee Mungu uliye mwadilifu,uzijuaye siri za mioyo na fikira za watu.

10. Mungu ndiye ngao yangu;yeye huwaokoa wanyofu wa moyo.

11. Mungu ni hakimu wa haki;kila siku hulaumu maovu.

12. Watu wasipoongoka,Mungu atanoa upanga wake;atavuta upinde wake na kulenga shabaha.

13. Atatayarisha silaha zake za hatari,na kuipasha moto mishale yake.

14. Tazama! Mtu mbaya hutunga uovu,hujaa uharibifuna kuzaa udanganyifu.

Kusoma sura kamili Zaburi 7