Agano la Kale

Agano Jipya

Zaburi 7:8-14 Biblia Habari Njema (BHN)

8. Wewe, ee Mwenyezi-Mungu, wayahukumu mataifa;unihukumu kadiri ya uadilifu wangu,kulingana na huo unyofu wangu.

9. Uukomeshe uovu wa watu wabaya,uwaimarishe watu walio wema,ee Mungu uliye mwadilifu,uzijuaye siri za mioyo na fikira za watu.

10. Mungu ndiye ngao yangu;yeye huwaokoa wanyofu wa moyo.

11. Mungu ni hakimu wa haki;kila siku hulaumu maovu.

12. Watu wasipoongoka,Mungu atanoa upanga wake;atavuta upinde wake na kulenga shabaha.

13. Atatayarisha silaha zake za hatari,na kuipasha moto mishale yake.

14. Tazama! Mtu mbaya hutunga uovu,hujaa uharibifuna kuzaa udanganyifu.

Kusoma sura kamili Zaburi 7