Agano la Kale

Agano Jipya

Zaburi 7:1-5 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Ee Mwenyezi-Mungu, Mungu wangu, nakimbilia usalama kwako;uniokoe na wote wanaonidhulumu, unisalimishe.

2. La sivyo, watakuja kunirarua kama simba,wakanivutia mbali, pasiwe na wa kuniokoa.

3. Ee Mwenyezi-Mungu, Mungu wangu!Kama nimetenda moja ya mambo haya:Kama nimechafua mikono yangu kwa ubaya,

4. kama nimemlipa rafiki yangu mabaya badala ya mema,au nimemshambulia adui yangu bila sababu,

5. basi, adui na anifuatie na kunikamata;ayakanyage maisha yangu;na kuniulia mbali.

Kusoma sura kamili Zaburi 7