4. Uitafute furaha yako kwa Mwenyezi-Mungu,naye atakujalia unayotamani moyoni.
5. Mkabidhi Mwenyezi-Mungu maisha yako;mtumainie yeye naye atafanya kitu.
6. Ataufanya wema wako ungae kama mwanga,na uadilifu wako kama jua la adhuhuri.
7. Tulia mbele ya Mwenyezi-Mungu, mngojee kwa saburi;usihangaike juu ya wale wanaofanikiwa,watu wanaofaulu katika mipango yao mibaya.
8. Epuka hasira wala usiwe na ghadhabu;usihangaike maana hiyo huzidisha ubaya.
9. Watu watendao mabaya wataangamizwa,bali wanaomtumaini Mwenyezi-Mungu wataimiliki nchi.
10. Bado kitambo kidogo, naye mwovu atatoweka;utamtafuta pale alipokuwa, wala hutamwona.
11. Lakini wapole wataimiliki nchi,hao watafurahia wingi wa fanaka.
12. Mwovu hula njama dhidi ya mwadilifu,na kumsagia meno kwa chuki.
13. Lakini Mwenyezi-Mungu humcheka mwovu,kwani ajua mwisho wake u karibu.
14. Waovu huchomoa panga na kuvuta pinde zao,wapate kuwaua maskini na fukara;wawachinje watu waishio kwa unyofu.
15. Lakini panga zao zitawapenya wao wenyewe,na pinde zao zitavunjwavunjwa.