Agano la Kale

Agano Jipya

Zaburi 37:35-40 Biblia Habari Njema (BHN)

35. Nilimwona mwovu mdhalimu sana,alijiweka juu ya wote kama mierezi ya Lebanoni!

36. Baadaye nikapita hapo, naye hakuwapo tena;nikamtafuta, lakini hakuonekana tena.

37. Mwangalie mtu mwema, mtu mwadilifu;mtu anayependa amani hujaliwa wazawa.

38. Lakini wakosefu wote wataangamizwa;na wazawa wao watafutiliwa mbali.

39. Mwenyezi-Mungu huwaokoa waadilifu,na kuwalinda wakati wa taabu.

40. Mwenyezi-Mungu huwasaidia na kuwaokoa;huwatoa makuchani mwa waovu na kuwaokoa,maana wanakimbilia usalama kwake.

Kusoma sura kamili Zaburi 37