Agano la Kale

Agano Jipya

Zaburi 37:30-34 Biblia Habari Njema (BHN)

30. Mtu mwadilifu husema maneno ya hekima,kwa ulimi wake hunena yaliyo ya haki.

31. Huizingatia moyoni mwake sheria ya Mungu wake;naye hatetereki katika mwenendo wake.

32. Mtu mwovu humvizia mtu mwema na kujaribu kumuua;

33. lakini Mwenyezi-Mungu hatamtia mtu mwema makuchani mwake,wala kumwacha apatilizwe akishtakiwa.

34. Mtumainie Mwenyezi-Mungu na kushika njia yake,naye atakukuza uimiliki nchi,na kuwaona waovu wakiangamizwa.

Kusoma sura kamili Zaburi 37