30. Mtu mwadilifu husema maneno ya hekima,kwa ulimi wake hunena yaliyo ya haki.
31. Huizingatia moyoni mwake sheria ya Mungu wake;naye hatetereki katika mwenendo wake.
32. Mtu mwovu humvizia mtu mwema na kujaribu kumuua;
33. lakini Mwenyezi-Mungu hatamtia mtu mwema makuchani mwake,wala kumwacha apatilizwe akishtakiwa.
34. Mtumainie Mwenyezi-Mungu na kushika njia yake,naye atakukuza uimiliki nchi,na kuwaona waovu wakiangamizwa.