Agano la Kale

Agano Jipya

Zaburi 37:27-40 Biblia Habari Njema (BHN)

27. Achana na uovu, utende mema,nawe utaishi nchini daima;

28. maana Mwenyezi-Mungu hupenda uadilifu,wala hawaachi waaminifu wake.Huwalinda hao milele;lakini wazawa wa waovu wataangamizwa.

29. Waadilifu wataimiliki nchi,na wataishi humo milele.

30. Mtu mwadilifu husema maneno ya hekima,kwa ulimi wake hunena yaliyo ya haki.

31. Huizingatia moyoni mwake sheria ya Mungu wake;naye hatetereki katika mwenendo wake.

32. Mtu mwovu humvizia mtu mwema na kujaribu kumuua;

33. lakini Mwenyezi-Mungu hatamtia mtu mwema makuchani mwake,wala kumwacha apatilizwe akishtakiwa.

34. Mtumainie Mwenyezi-Mungu na kushika njia yake,naye atakukuza uimiliki nchi,na kuwaona waovu wakiangamizwa.

35. Nilimwona mwovu mdhalimu sana,alijiweka juu ya wote kama mierezi ya Lebanoni!

36. Baadaye nikapita hapo, naye hakuwapo tena;nikamtafuta, lakini hakuonekana tena.

37. Mwangalie mtu mwema, mtu mwadilifu;mtu anayependa amani hujaliwa wazawa.

38. Lakini wakosefu wote wataangamizwa;na wazawa wao watafutiliwa mbali.

39. Mwenyezi-Mungu huwaokoa waadilifu,na kuwalinda wakati wa taabu.

40. Mwenyezi-Mungu huwasaidia na kuwaokoa;huwatoa makuchani mwa waovu na kuwaokoa,maana wanakimbilia usalama kwake.

Kusoma sura kamili Zaburi 37