Agano la Kale

Agano Jipya

Zaburi 37:23-28 Biblia Habari Njema (BHN)

23. Mwenyezi-Mungu huziongoza nyayo za mtu,humlinda yule ampendezaye.

24. Ajapoanguka, haanguki akabaki chini,kwa sababu Mwenyezi-Mungu humtegemeza.

25. Nilikuwa kijana na sasa ni mzee;kamwe sijaona mwadilifu ameachwa na Mungu,au watoto wake wakiombaomba chakula.

26. Daima huwapa wengine kwa furaha na kukopesha,na watoto wake ni baraka.

27. Achana na uovu, utende mema,nawe utaishi nchini daima;

28. maana Mwenyezi-Mungu hupenda uadilifu,wala hawaachi waaminifu wake.Huwalinda hao milele;lakini wazawa wa waovu wataangamizwa.

Kusoma sura kamili Zaburi 37