Agano la Kale

Agano Jipya

Zaburi 37:2-12 Biblia Habari Njema (BHN)

2. Maana hao watatoweka mara kama nyasi;watanyauka kama mimea mibichi.

3. Mtumainie Mwenyezi-Mungu na kutenda mema,upate kuishi katika nchi na kuwa salama.

4. Uitafute furaha yako kwa Mwenyezi-Mungu,naye atakujalia unayotamani moyoni.

5. Mkabidhi Mwenyezi-Mungu maisha yako;mtumainie yeye naye atafanya kitu.

6. Ataufanya wema wako ungae kama mwanga,na uadilifu wako kama jua la adhuhuri.

7. Tulia mbele ya Mwenyezi-Mungu, mngojee kwa saburi;usihangaike juu ya wale wanaofanikiwa,watu wanaofaulu katika mipango yao mibaya.

8. Epuka hasira wala usiwe na ghadhabu;usihangaike maana hiyo huzidisha ubaya.

9. Watu watendao mabaya wataangamizwa,bali wanaomtumaini Mwenyezi-Mungu wataimiliki nchi.

10. Bado kitambo kidogo, naye mwovu atatoweka;utamtafuta pale alipokuwa, wala hutamwona.

11. Lakini wapole wataimiliki nchi,hao watafurahia wingi wa fanaka.

12. Mwovu hula njama dhidi ya mwadilifu,na kumsagia meno kwa chuki.

Kusoma sura kamili Zaburi 37