17. Maana nguvu za waovu zitavunjwa,lakini Mwenyezi-Mungu huwategemeza waadilifu.
18. Mwenyezi-Mungu hutunza maisha ya watu waaminifu,na urithi wao utadumu milele.
19. Hawataaibika zikifika nyakati mbaya;siku za njaa watakuwa na chakula tele.
20. Lakini waovu wataangamia,maadui za Mwenyezi-Mungu watanyauka kama maua nyikani;naam, watatoweka kama moshi.
21. Mtu mwovu hukopa bila kurudisha;lakini mwadilifu hutoa kwa ukarimu.
22. Waliobarikiwa na Mwenyezi-Mungu wataimiliki nchi,lakini waliolaaniwa naye watafutiliwa mbali.