1. Usihangaike kwa sababu ya waovu;usiwaonee wivu watendao mabaya.
2. Maana hao watatoweka mara kama nyasi;watanyauka kama mimea mibichi.
3. Mtumainie Mwenyezi-Mungu na kutenda mema,upate kuishi katika nchi na kuwa salama.
4. Uitafute furaha yako kwa Mwenyezi-Mungu,naye atakujalia unayotamani moyoni.
5. Mkabidhi Mwenyezi-Mungu maisha yako;mtumainie yeye naye atafanya kitu.
6. Ataufanya wema wako ungae kama mwanga,na uadilifu wako kama jua la adhuhuri.