19. Usiwaache maadui hao wabaya wanisimange,hao wanichukiao bure wafurahie mateso yangu.
20. Maneno wasemayo si ya amani,wanazua maneno ya hila dhidi ya wananchi watulivu.
21. Wananishtaki kwa sauti:“Haya! Haya! Tumeona wenyewe uliyotenda!”
22. Lakini wewe Mwenyezi-Mungu waona jambo hilo,usinyamaze, ee Mwenyezi-Mungu,usikae mbali nami.
23. Uinuke, ee Mwenyezi-Mungu, ukanitetee;uje, ee Mungu wangu, uangalie kisa changu.