Agano la Kale

Agano Jipya

Zaburi 35:1-7 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Ee Mwenyezi-Mungu, uwapinge hao wanaonipinga;uwashambulie hao wanaonishambulia.

2. Utwae ngao yako na kingio lako,uinuke uje ukanisaidie!

3. Chukua mkuki na sime yako dhidi ya wanaonifuatia.Niambie mimi kwamba utaniokoa.

4. Waone haya na kuaibika,hao wanaoyanyemelea maisha yangu!Warudishwe nyuma kwa aibu,hao wanaozua mabaya dhidi yangu.

5. Wawe kama makapi yapeperushwayo na upepo,wakikimbizwa na malaika wa Mwenyezi-Mungu!

6. Njia yao iwe ya giza na utelezi,wakifukuzwa na malaika wa Mwenyezi-Mungu!

7. Maana walinitegea mitego bila sababu;walinichimbia shimo bila kisa chochote.

Kusoma sura kamili Zaburi 35