2. Unitegee sikio, uniokoe haraka!Uwe kwangu mwamba wa usalama,ngome imara ya kuniokoa.
3. Naam, wewe ni mwamba wangu na ngome yangu;kwa hisani yako uniongoze na kunielekeza.
4. Unitoe katika mtego walionitegea mafichoni;maana wewe ni kimbilio la usalama wangu.
5. Mikononi mwako naiweka roho yangu;umenikomboa, ee Mwenyezi-Mungu, Mungu mwaminifu.
6. Wawachukia wanaoabudu sanamu batili;lakini mimi nakutumainia wewe, ee Mwenyezi-Mungu.
7. Nitashangilia na kufurahia fadhili zako,maana wewe waiona dhiki yangu,wajua na taabu ya nafsi yangu.
8. Wewe hukuniacha nitiwe mikononi mwa maadui zangu;umenisimamisha mahali pa usalama.
9. Unionee huruma, ee Mwenyezi-Mungu, niko taabuni;macho yangu yamechoka kwa huzuni,nimeishiwa nguvu mwilini na rohoni.
10. Maisha yangu yamekwisha kwa majonzi;naam, miaka yangu kwa kulalamika.Nguvu zangu zimeniishia kwa kutaabika;hata mifupa yangu imekauka.
11. Nimekuwa dharau kwa maadui zangu wote;kioja kwa majirani zangu.Rafiki zangu waniona kuwa kitisho;wanionapo njiani hunikimbia.
12. Nimesahaulika kama mtu aliyekufa;nimekuwa kama chungu kilichovunjikavunjika.
13. Nasikia watu wakinongonezana,vitisho kila upande;wanakula njama dhidi yangu,wanafanya mipango ya kuniua.
14. Lakini mimi nakutumainia wewe, ee Mwenyezi-Mungu.Nasema: “Wewe ni Mungu wangu!”