1. Kwako, ee Mwenyezi-Mungu, nakimbilia usalama,usiniache niaibike kamwe;kwa uadilifu wako uniokoe.
2. Unitegee sikio, uniokoe haraka!Uwe kwangu mwamba wa usalama,ngome imara ya kuniokoa.
3. Naam, wewe ni mwamba wangu na ngome yangu;kwa hisani yako uniongoze na kunielekeza.
4. Unitoe katika mtego walionitegea mafichoni;maana wewe ni kimbilio la usalama wangu.
5. Mikononi mwako naiweka roho yangu;umenikomboa, ee Mwenyezi-Mungu, Mungu mwaminifu.