Agano la Kale

Agano Jipya

Zaburi 31:1-5 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Kwako, ee Mwenyezi-Mungu, nakimbilia usalama,usiniache niaibike kamwe;kwa uadilifu wako uniokoe.

2. Unitegee sikio, uniokoe haraka!Uwe kwangu mwamba wa usalama,ngome imara ya kuniokoa.

3. Naam, wewe ni mwamba wangu na ngome yangu;kwa hisani yako uniongoze na kunielekeza.

4. Unitoe katika mtego walionitegea mafichoni;maana wewe ni kimbilio la usalama wangu.

5. Mikononi mwako naiweka roho yangu;umenikomboa, ee Mwenyezi-Mungu, Mungu mwaminifu.

Kusoma sura kamili Zaburi 31